Pages

Saturday, August 17, 2013

DORICE MOLLEL NDIYE REDD'S MISS ILALA 2013

Redds Miss Ilala  Dorice Mollel (katikati) akiwa na washindi wenzake, kulia ni mshindi wa pili Alice Isaac na kushoto mshindi wa tatu Clara Bayo.




************************

Miss Tabata  Dorice Mollel (22) usiku wa kuamkia jana aliwashinda warembo wengine 13 katika shindano la kumtafuta Redd's Miss Ilala 2013 lililofanyika katika ukumbi wa Golden Jubilee Tower, Dar es Salaam na kufanikiwa kumrithi Noela Michael ambaye alishinda taji hilo mwaka jana, pia akitokea Tabata.

Dorice alizawadiwa shilingi 1.5 milioni/-, na mshindi wa pili Alice Isaac (Dar City Centre) alipata shilingi 1 milioni /-.

Mshindi wa tatu katika shindamo hilo ni Clara Bayo (Dar City Centre) ambaye  alizawadiwa  Sh. 700,000/-. Mshindi wanne Pendo Lema (Tabata) alizawadiwa Sh. 400,000/- na wa tano  Shamim Mohamed alipata Sh. 300,000/-.

Mrembo Juanita Kabunga kutoka Tabata alizawadiwa Sh. 500,000/- baada ya kushinda Miss Talent na Kabula Kibogoti pia kutoka Tabata alishinda taji la Miss Rio and Spa na kuzawadiwa Sh. 200,000/- na ajira ya kudumu kwenye kampuni hiyo.

Warembo waliosalia kila moja alipata kifuta jasho cha Sh. 200,000/- ambao ni Clara Paul, Anna Johnson, Irene Mwelolo, Rehema Mpanda,  Martha Gewe, Diana Joachim, Natasha Mohamed,  Kazumbe Mussa, Kabula Kibogoti na Juanita Kabunga.

No comments: