Pages

Saturday, August 17, 2013

FAMILIA ZA JAMII MASIKINI ZAFURAHIA MRADI WA KUKU CHINI YA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA KIMAREKANI LA HEIFER INTERNATIONAL

Mfugaji wa kuku wa asili Bw.  Nicodemus Nzenga mkazi wa kijiji cha  Maluwe akionyesha vifaranga ambavyo vimetotolewa na kuku wa asili ambao anawafuga kupitia mradi wa kuku wa shirika la kimataifa la Kimarekani la Heifer International.
   
Mtaalamu wa mifugo wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa  Bw. Nicodemus Nzenga (kulia) akimwelekeza jambo mfugaji wa kuku wa asili mkazi wa kijiji cha  Maluwe Bw. Abdalla Salum.  Mradi huo umefadhiliwa na Shirika la kimataifa la Kimarekani la Heifer International.
     
Bi Asha Ramadhani mfugaji wa kuku wa asili wa kijiji cha Zombo wilayani Kilosa mkoani Morogoro, akiwa amemkamata mmoja wa kuku anaowafuga kupitia mradi wa ufugaji kuku unaofadhiliwa na Shirika la kimataifa la Kimarekani la Heifer International.


FAMILIA ZA JAMII MASIKINI ZINAZOISHI KATIKA VIJIJI VYA MALUWE NA ZOMBO VILIVYOPO KATIKA WILAYA YA KILOSA MKOANI MOROGORO ZIMESEMA KUWA MRADI WA KUKU WA ASILI CHINI YA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA KIMAREKANI LA HEIFER PAMOJA NA MAFUNZO WALIYO YAPATA YA UFUGAJI WA KUKU HAO KWA MBINU ZA KISASA  UNAWEZA KUWASAIDIA KUWATOA KATIKA WIMBI LA UMASIKI LINALO WAKABILI KWA MUDA MREFU SASA.

WAKAZI HAO WAKIZUNGUMZA KWA NYAKATI TOFAUTI KATIKA VIJIJI HIVYO WAMESEMA KUWA HALI YA MAISHA YAO NI DUNI NA WANATEGEMEA KILIMO PEKEE AMBACHO KWA MUDA MREFU HAKIJASAIDIA KATIKA KUINUA PATO LAO NA HIVYO KUENDELEA KUBAKI MASIKINI AMBAPO WAMEFAFANUA KWAMBA WANA IMANI KUPITIA MRADI HUO WA UFUGAJI WA KUKU WA ASILI KWA MBINU ZA KISASA KUTAWEZA KUWASAIDIA KUBADILISHA MAISHA YAO KUTOKANA NA MAUZO YA KUKU HAO.

BWANA NICODEMUS NZENGA AMBAYE NI MTAALAMU WA MIFUGO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA NA MRATIBU WA MIRADI YA HEIFER WILAYANI HAPO AMEPONGEZA JITIHADA ZINAZOFANYWA NA SHIRIKA HILO AMBAPO AMEELEZEA KUWA CHANGAMOTO BADO NI KUBWA KUTOKANA NA UHITAJI MKUBWA UNAOTOKANA NA KUWEPO KWA FAMILIA NYINGI ZENYE SHIDA AMBAPO SHIRIKA HILO LIMEKUWA LIKISAIDIA JAMII MASIKINI 285 KUTOKA VIJIJI 14 TU KATI YA 161 VILIVYOPO KATIKA WILAYA HIYO.

No comments: