Pages

Wednesday, March 27, 2013

ASASI YA VIJANA YA UMOJA WA MATAIFA TANZANIA KUANDAA BARAZA KUU KIVULI LA KIMATAIFA LA UMOJA WA MATAIFA



Mwenyekiti wa Asasi ya vijana ya Umoja wa Mataifa-YUNA akizungumza na waandishi wa  Habari hawapo pichani  kushoto kwake ni Bi Catherine Fidelis Mwenyekiti wa Baraza kivuli la Umoja wa Mataifa -TIMUN 2013

Baadhi ya Wajumbe wa YUNA wakiwa katika picha ya pamoja katika mkutano na Wandishi wa habari uliofanyika idara ya habari Maelezo  jijini Dar es Salaam.



Baadhi ya sehemu ya waandishi wa Habari ambao wamehudhuria  mkutano  wa YUNA na Waandishi wa  HAbari


Picha ya juu na chini Baadhi ya waandishi wa habari wakikamilisha taarifa zao mara baada mkutano na  viongozi wa  YUNA 


Du unaona tumemaliza una la kuongeza Mwenyekiti wa YUNA na TIMUN mara  baada ya  kumaliza  mkutano na  Wandishi wa Habari.
 Kama tunavyofahamu, tunaelekea mwishoni mwa Malengo ya Maendeleo ya Kimilenia, Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa Tanzania imeanza harakati za majadiliano ya mikakati baada ya 2015 kati ya vijana kwenye zaidi ya mikoa sita nchini Tanzania.

Mwaka huu, mkutano wa Baraza Kuu Kivuli La Kimataifa la Umoja wa Mataifa litafanyika Dodoma katika ukumbi wa bunge wa Pius Msekwa kuanzia tarehe 2 hadi 6 Aprili 2013 ikiwa na mada isemayo, “Malengo ya Maendeleo ya Kimilenia, kutazama mikakati ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi baada ya 2015”.

Mkutano huu utashirikisha vijana 160 waliochaguliwa kutoka Tanzania bara na visiwani pamoja na vijana kutoka nchi mbalimbali duniani. Lengo letu kuu ni kuhakikisha kwamba sauti ya vijana inahusishwa katika ajenda za mashauriano ya Malengo ya Maendeleo ya Kimilenia na kuandaa ripoti ambayo itajumuishwa katika taarifa ya taifa itakayopelekwa kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Mkutano huu wa kimataifa utakuwa majadiliano ya mwisho ya vijana kabla ya kutayarisha taarifa ya mwisho.

Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa Tanzania inayofuraha kuwajulisha kwamba, mwaka huu Tanzania itakuwa mwenyeji wa mkutano wa Baraza Kuu Kivuli La Kimataifa la Umoja wa Mataifa. Kwa miaka kumi na tano, Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa imekuwa ikiandaa mkutano wa Baraza Kuu Kivuli la Umoja wa Mataifa, ambapo washiriki hupata fursa ya kufanya kazi kama wanadiplomasia na hushiriki katika vipindi sawa na vile vya mashirika ya kiserikali. Washiriki hufanya utafiti kuhusu nchi fulani, hupata majukumu kama yale ya wanadiplomasia, hufanya utafiti wa masuala ya kimataifa, hujadili, huelimishana, hushauriana na hatimaye kupendekeza masuluhisho ya matatizo mbalimbali ya dunia.

Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa Tanzania inapenda kutumia fursa hii kukaribisha Watanzania wote kuungana mkono na vijana wa Tanzania watakavyokuwa wanatoa michango na mitazamo yao mikubwa na ya kimataifa katika suala la ajenda ya malengo ya maendeleo ya kimilenia baada ya 2015.

Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa Tanzania pia inachukua nafasi hii kuwaomba mashirika ya  kiserikali na yasiyo ya kiserikali kuwa kipaombele katika kuwasaidia vijana wanaposhiriki katika nafasi hii ya pekee inayokusudia kuwaleta vijana wa Tanzania karibu na Umoja wa Mataifa pamoja na dunia kwa ujumla.





No comments: