Pages

Wednesday, March 27, 2013

MUDA WA KUREJESHA FOMU ZA PROGRAMU YA –SAFARI LAGER WEZESHWA WAONGEZWA.


Meneja wa bia ya Safari Lager Bw Oscar Shelukindo akiwaonyesha Waandishi wa  Habari  Hawapo pichani  tovuti maalumu kwa ajili ya programu ya Safari Wezeshwa


Joseph Migunda mwenye fulana nyeusi akisisitiza jambo katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika  katika kiwanda cha bia TBL jijini Dar es Salaam  anayemfuatia kulia kwake ni Oscar Shelukindo Meneje wa Safari Lager na Lawrence Mratibu wa programu hiyo kutoka kampuni ya intergrated communicatins. 

Oscar Shelukindo meneja wa bia ya Safari akizunguza na waandishi wa Habari hawapo pichani



Oscar akionyesha mtando wa  programe ya Safari wezeshwa (picha zote na IPSHA MEDIA)


Hatimaye muda wa kurejesha fomu za progmu ya SAFARI LAGER WEZESHWA umeongezwa mpaka kufiki tarehe 15 mwezi wa 4 kutokana na maombi ya wajasiriamali wengi ambao hawakuweza kupata fomu hizo kwa wakati.

Akizungumza na jijini Dar es salaam leo meneja wa bia ya Safari lager Oscar Shelukindo amesema kuwa nia hasa ya Safari Lagel ni kuhakikisha kuwa inawawezesha wajasiriamali kutimiza ndoto zao.

Amesema milioni 200 zimetengwa kwa ajili ya kuwasaidia wajasiriamali kwa ajili ya kuwasaidia vitendea kazi na kuongeza kuwa kutokana na maombi yao wameamua kusogeza mbele siku za kurudisha fona na kuwataka wachangamkie nafasi hiyo.

Naye jaji mkuu wa program hiyo Bw Joseph Migunda kutoka taasisi Ya TAPBDS   amesema kuwa sifa za kushiriki program hiyo ni sawa na mwaka jana na kuongeza kuwa washiriki wana takiwa kuwa na sifa kuu nne ikiwemo wawe wachapakazi, biashara zao ziwe halali, wawe na umri kati ya miaka 18 mpaka 40 na wawe na nia za kukuza biashara zao.


No comments: