![]() |
| Msanii wa Bongo Movie, Jackob Steven a.k.a. JB. |
MKALI wa Bongo Movie Tanzania Jocob Steven maarufu kama JB amesema kwamba marehemu Kanumba alikuwa mzuri katika kuigiza ‘Movie’ ila bado kuna watu wanafanya vizuri zaidi ya pale alipopaacha.
JB amesema hayo leo mchana kupitia Planet Bongo ya East Africa Radio, kwamba kuifanya akili ya binadamu kusahau kitu alichokiacha msanii aliyekuwa juu sio kazi rahisi.

JB amesema hayo leo mchana kupitia Planet Bongo ya East Africa Radio, kwamba kuifanya akili ya binadamu kusahau kitu alichokiacha msanii aliyekuwa juu sio kazi rahisi.

Marehemu Steven Kanumba, enzi za uhai wake.
Msanii huyo ametoa mfano wa aliyekuwa
mkali wa Filamu za mapigano na Karate duniani Bluce Lee, ambaye
alifariki wakati yupo katika kiwango cha hali ya juu, leo ukimueleza mtu
kwamba Jackie Chan anafanya vizuri zaidi yake atakataa.
”Kanumba alifanya vizuri kwa muda
mchache sana kisha Mungu akamchukua, wakati anafanya vizuri ndio hapo
hapo mshumaa ukazima, sio rahisi kumuaminisha mtu kwa kiwango
alichofanya Kanumba na alipoishia kuweza kufananisha na sasa kwakuwa
alifanya vizuri zaidi ila bado waliopo wanafanya vizuri,” amesema JB.
JB ameongeza kuwa Kanumba alikifikisha
Kiwanda cha Filamu pazuri kwa kiwango chake, ila kila ‘Industry’ kuna
wakati inapanda wakati mwingine inashuka na anaamini sasa wunarudi
vizuri.

No comments:
Post a Comment