
Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu imeamuru washtakiwa wa kesi ya mauaji ya Aneth Msuya,
wakatibiwe baada ya kukubaliana na madai yao kuwa walipigwa wakiwa
mahabusu katika kituo cha Polisi.
Washtakiwa hao
Miriam Mrita (41) na mfanyabiashara Revocatus Muyela (40), wanadaiwa
kumuua Aneth, ambaye ni dada wa bilionea Erasto Msuya kwa kumchinja
akiwa nyumbani kwake, Kibada Kigamboni mei 25, 2016.
Mariam ambaye ni
mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ni mjane wa bilionea Msuya,
aliyekuwa mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite. Bilionea Msuya pia
aliuawa kwa kupigwa risasi Agosti 2015 eneo la Mijohoroni, kando mwa
barabara ya Arusha – Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Uamuzi wa Mahakama
kwa washtakiwa kwenda kutibiwa unatokana na malalamiko yao
waliyoyatoa kupitia kwa Wakili Peter Kibatala kuwa walipokuwa
mahabusu, waliteswa kwa kupigwa na kulazimishwa kukubali kutenda kosa
hilo katika maelezo yao.
Mbali na madai ya
washtakiwa hao kuteswa na kuomba Mahakama ifanye uchunguzi na iagize
watibiwe, pia Wakili Kibatala alidai hati ya madai ina kasoro za
kisheria.
Mahakama ya Kisutu
katika uamuzi wake uliotolewa na Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa
ilikubaliana na madai ya washtakiwa hao.
No comments:
Post a Comment