Dodoma na Mtwara.
Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na mapigano kati ya wakulima na wafugaji katika Hifadhi ya Embroi Murtangosi, wilayani Kiteto mkoani Manyara, imefikia 10.
Wakati hayo yakiendelea, huko Mtwara askari polisi wawili na raia mmoja wameuawa kwa kupigwa risasi na jambazi. Kuongezeka kwa idadi ya waliokufa huko Kiteto, kunafuatia kupatikana kwa miili ya watu wengine watatu katika Kitongoji cha Mtanzania. Awali ilielezwa kuwa watu sita walikuwa wameuawa katika mapigano hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Martha Umbulla, alisema watu hao watatu wamefariki dunia jana baada ya kushambuliwa na wafugaji wa jamii ya Kimasai.
Alisema “hali ya usalama katika hifadhi hiyo, bado haijatengemaa na kwamba watu wanaendelea kukimbia.”
Mkuu huyo wa wilaya alisema alifika katika kitongoji hicho na kushuhudia miili ya watu hao ambao kwa sasa wamehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto ikisubiri kutambuliwa. Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima na Wafugaji wilayani humo (Chawaki), Hassan Losiyoki, alisema hali si shwari na kwamba watu bado wanauawa.
Mapigano hayo yamedumu kwa miaka minane na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 20 na wengine 14 kujeruhiwa.
Kutoka Mtwara. Abdallah Nasoro anaaripoti kuwa watu watatu wakiwamo askari polisi wawili wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi katika Wilaya ya Newala. mwingine, amevunjwa kiuno.
Habari zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen, zilisema tukio hilo lilitokea juzi jioni katika Msitu wa Kijiji cha Kiduni, ambako majambazi yalikimbilia baada ya kupora fedha kutoka kwenye kituo cha mafuta kilichopo katika kijiji hicho. Habari hizo zilisema katika tukio hilo, majambazi walimuua mwananchi mmoja kwa kumpiga risasi kisha kupora fedha ambazo hazijafahamika ni kiasi gani na kutokomea msituni.
Kwa mujibu wa habari hizo, polisi waliwafuta majambazi hayo na kuanza kujibizana kwa risasi.
Inasemekana wakati wakiendelea na mapambano jambazi mmoja alitokomea na kumwacha mmoja ambaye alikuwa na silaha mkononi akiendelea na mapambano.
Baadaye jambazi huyo alinyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha na ndipo askari wawili walipomfuata kwa lengo la kumkamata, lakini ghafla alichukua silaha yake na kuwafyatulia risasi na kufa papo hapo.
Imeelezwa kuwa katika harakati za kuokoa maisha yake askari mmoja ambaye alikuwa dereva wa gari la polisi, alipigwa risasi ya kiuononi na kusababisha kuvunjika kwa sehemu hiyo ya mwili.
Habari zinasema polisi wanaendelea na msako dhidi ya majambazi hao.
Wakati hayo yakiendelea, huko Mtwara askari polisi wawili na raia mmoja wameuawa kwa kupigwa risasi na jambazi. Kuongezeka kwa idadi ya waliokufa huko Kiteto, kunafuatia kupatikana kwa miili ya watu wengine watatu katika Kitongoji cha Mtanzania. Awali ilielezwa kuwa watu sita walikuwa wameuawa katika mapigano hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Martha Umbulla, alisema watu hao watatu wamefariki dunia jana baada ya kushambuliwa na wafugaji wa jamii ya Kimasai.
Alisema “hali ya usalama katika hifadhi hiyo, bado haijatengemaa na kwamba watu wanaendelea kukimbia.”
Mkuu huyo wa wilaya alisema alifika katika kitongoji hicho na kushuhudia miili ya watu hao ambao kwa sasa wamehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto ikisubiri kutambuliwa. Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima na Wafugaji wilayani humo (Chawaki), Hassan Losiyoki, alisema hali si shwari na kwamba watu bado wanauawa.
Mapigano hayo yamedumu kwa miaka minane na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 20 na wengine 14 kujeruhiwa.
Kutoka Mtwara. Abdallah Nasoro anaaripoti kuwa watu watatu wakiwamo askari polisi wawili wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi katika Wilaya ya Newala. mwingine, amevunjwa kiuno.
Habari zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen, zilisema tukio hilo lilitokea juzi jioni katika Msitu wa Kijiji cha Kiduni, ambako majambazi yalikimbilia baada ya kupora fedha kutoka kwenye kituo cha mafuta kilichopo katika kijiji hicho. Habari hizo zilisema katika tukio hilo, majambazi walimuua mwananchi mmoja kwa kumpiga risasi kisha kupora fedha ambazo hazijafahamika ni kiasi gani na kutokomea msituni.
Kwa mujibu wa habari hizo, polisi waliwafuta majambazi hayo na kuanza kujibizana kwa risasi.
Inasemekana wakati wakiendelea na mapambano jambazi mmoja alitokomea na kumwacha mmoja ambaye alikuwa na silaha mkononi akiendelea na mapambano.
Baadaye jambazi huyo alinyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha na ndipo askari wawili walipomfuata kwa lengo la kumkamata, lakini ghafla alichukua silaha yake na kuwafyatulia risasi na kufa papo hapo.
Imeelezwa kuwa katika harakati za kuokoa maisha yake askari mmoja ambaye alikuwa dereva wa gari la polisi, alipigwa risasi ya kiuononi na kusababisha kuvunjika kwa sehemu hiyo ya mwili.
Habari zinasema polisi wanaendelea na msako dhidi ya majambazi hao.
No comments:
Post a Comment