Wanasayansi wanadai kuunda aina ya ngozi inayoweza kubandikwa juu ya mwili wa mtu kupunguza muonekano wa mikunjo ya ngozi mwilini na ngozi inayopwaya chini ya macho kutokana na uzee.
Ni aina ya maji maji mtu anayopaka mwilini alafu inaachwa kukauka ambapo baadaye huishia kuwa ngozi nyembamba iliyo mithili ya 'ngozi ya ujana,' Nature Materials inaarifu baada ya kufanya majiribio kadhaa madogo.
Kwa sasa inafanyiwa majaribio ya kuuzwa kama bidhaa ya urembo.
Lakini wanasayansi Marekani wanasema "ngozi ya pili" huenda baadaye ikaweza kutumika kutengeneza dawa na kinga dhidi ya jua.
Ngozi ya pili
Kundi la wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Havard kitengo cha matibabu na Taasisi ya teknolojia Massachusetts wamefanya majaribio ya bidhaa hiyo kwa watu waliojitolea ambao walipakwa ngozi hiyo chini ya macho, kwenye mikono yao na miguu.
Ngozi hiyo inayotokana na kemikali polysiloxane polymer iliundwa kwenye maabara kwa kutumia chembe chembe za Silicone na hewa safi ya Oxygen.
Licha ya kwamba sio ngozi ya kweli lakini imeundwa kuiga ngozi asili na pia kuacha nafasi ya hewa kupita.
Kwa mujibu wa watafiti ngozi hiyo bandia ina uwezo wa kunasa mvuke na kusaidia ngozi kujivuta kiasi cha inavyostahili.
Ni aina ya maji maji mtu anayopaka mwilini alafu inaachwa kukauka ambapo baadaye huishia kuwa ngozi nyembamba iliyo mithili ya 'ngozi ya ujana,' Nature Materials inaarifu baada ya kufanya majiribio kadhaa madogo.
Kwa sasa inafanyiwa majaribio ya kuuzwa kama bidhaa ya urembo.
Lakini wanasayansi Marekani wanasema "ngozi ya pili" huenda baadaye ikaweza kutumika kutengeneza dawa na kinga dhidi ya jua.
Ngozi ya pili
Kundi la wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Havard kitengo cha matibabu na Taasisi ya teknolojia Massachusetts wamefanya majaribio ya bidhaa hiyo kwa watu waliojitolea ambao walipakwa ngozi hiyo chini ya macho, kwenye mikono yao na miguu.
Ngozi hiyo inayotokana na kemikali polysiloxane polymer iliundwa kwenye maabara kwa kutumia chembe chembe za Silicone na hewa safi ya Oxygen.
Licha ya kwamba sio ngozi ya kweli lakini imeundwa kuiga ngozi asili na pia kuacha nafasi ya hewa kupita.
Kwa mujibu wa watafiti ngozi hiyo bandia ina uwezo wa kunasa mvuke na kusaidia ngozi kujivuta kiasi cha inavyostahili.
Jicho la kushoto limebandikwa Polymer, la kulia halikubandikwa. |
Wakati ngozi ikizeeka inanyauka na kwa hivyo haitoi matokeo mazuri vile kwenye majaribio haya.
Watafiti wanasema ngozi hiyo bandia haionekani na inaweza kubandikwa kwa siku nzima bila kuwa na madhara yoyote na inaweza kuhimili vitu kama jasho na mvua.
Lakini utafitia zaidi unahitajika. Ni lazima pia wakaguzi watoe idhini kwamba ni salama kutumiwa.
Dr Tamara Griffiths wa muungano wa madaktari wa ngozi Uingereza anasema ngozi ya chini ya macho hupwaya au kufura kutokana na mkusanyiko wa mafuta katika sehemu hiyo inayohusishwa na uzee.
Licha ya kwamba ni hali ya kawaida lakini watu wengi hujaribu mbinu tofuati kuziondoa, wengine hata kufanyiwa upasuaji.
Dr Griffiths amesema: "matokeo ya ngozi ya polymer yanaonesha kuwa sawa na kufanyiwa upasuaji bila ya hatari za upasuaji . Utafiti zaidi unahitajika, lakini huu ni mtazamo mzuri ulio na matumaini makubwa kwa tatizo la wengi. Nitafuatilia maendeleo ya utafiti huu kwa makini."
Watafiti wanasema ngozi hiyo bandia haionekani na inaweza kubandikwa kwa siku nzima bila kuwa na madhara yoyote na inaweza kuhimili vitu kama jasho na mvua.
Lakini utafitia zaidi unahitajika. Ni lazima pia wakaguzi watoe idhini kwamba ni salama kutumiwa.
Dr Tamara Griffiths wa muungano wa madaktari wa ngozi Uingereza anasema ngozi ya chini ya macho hupwaya au kufura kutokana na mkusanyiko wa mafuta katika sehemu hiyo inayohusishwa na uzee.
Licha ya kwamba ni hali ya kawaida lakini watu wengi hujaribu mbinu tofuati kuziondoa, wengine hata kufanyiwa upasuaji.
Dr Griffiths amesema: "matokeo ya ngozi ya polymer yanaonesha kuwa sawa na kufanyiwa upasuaji bila ya hatari za upasuaji . Utafiti zaidi unahitajika, lakini huu ni mtazamo mzuri ulio na matumaini makubwa kwa tatizo la wengi. Nitafuatilia maendeleo ya utafiti huu kwa makini."
Chanzo: BBC Swahili
No comments:
Post a Comment