Pages

Wednesday, August 14, 2013

SERIKALI YATAHADHARISHWA KUTOKEA KWA MIFARAKANO KATI YA WAFUGAJI NA MAKABILA YA WAFUGAJI AMBAYO YAMEVAMIA KATIKA KIJIJI CHA ULAYA MBUYUNI

 Bi Sharifa Mustafa mkazi wa Ulaya Mbuyuni wilayani Kilosa mkoani Morogoro akionyesha Ng'ombe wake ambaye amepatiwa na shirika la kimataifa la Heifer kwa lengo la kujikwamua kiuchumi  

Dakta Zengo Mikomagwa Mshauri wa mifugo Heifer International akizungumza na waandishi katika kijiji cha Ulaya Mbuyuni wilayani Kilosa mkoani Morogoro kuhusu miradi inayoendeshwa na shirika hilo hapa nchini.


Wanakikundi wa Mshikamano ambao wamebahatika kupata Ng'ombe wa maziwa kutoka shirika la kimataifa la Heifer International(PICHA ZOTE NA IPSHA MEDIA).

SERIKALI IMETAHADHARISHWA KUTOKEA KWA MIFARAKANO KATI YA WAFUGAJI NA MAKABILA YA WAFUGAJI AMBAYO YAMEVAMIA KATIKA KIJIJI CHA ULAYA MBUYUNI KILICHOPO WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGO AMBAPO MIFUGO HIYO IMEKUWA IKIARIBU MAZAO YAO NA VYAZO VYA MAJI JAMBO AMBALO HAWATO WEZA KULIVUMIA LIENDELEE.

WAKIZUNGUMZA KIJIJINI HAPO WAKAZI WA ENEO HILO AMBAO WAPO KATIKA MRADI WA UFUGAJI WA NG'OMBE WA KISASA CHINI YA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA HEIFER INTERNATIONAL WAMESEMA KUWA KUTOKANA NA MIFUGO YA WAVAMIZI AMBAO WANAFUGA NG'OMBE WA KIENYEJI NA HIVYO KUSABABISHA UHARIBIFU MKUBWA HATA WAO WAKO HATARINI KUKOSA MAJANI YA MALISHO YA NG'OMBE WAO AMBAO HAWATOKI MABANDANI NA HIVYO KUIOMBA SERIKALI KUCHUKUA HATUA ZA HARAKA ZA KUWAONDOA WAVAMIZI HAO KATIKA KIJIJI CHAO ILI WASIENDELEE KUFANYA UHARIBIFU HUO.

AWALI AKIZUNGUMZIA TATIZO LA MALISHO YA MIFUGO MSHAURI WA MASUALA YA MIFUGO KUTOKA SHIRIKA LA HEIFER AMESEMA KUWA SHIRIKA LAKE LIMEKUWA LIKIFANYA JITIHADA MBALIMBALI ZA KUHAKIKISHA KUWA MIFUGO WANAYO WAPATIA WAFUGAJI HAO AMBAO PIA NI WAKULIMA INAPATA MALISHO BORA AMBAPO WAMEANZA KUWAPATIA MAFUNZO YA MRADI WA SUKUMA VUTA AMBAO  UNAWAWEZESHA WAFUGAJI HAO KULIMA MAZAO YAO NA MAJANI YA MALISHO KATIKA SHAMBA MOJA.

No comments: