![]() |
Kutokana na hali hiyo tunawatahadharisha watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hatarishi kuchukua tahadhari,” imesema sehemu ya taarifa hiyo. (PICHA MAKTABA ) |
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa tahadhari ya kutokea kwa upepo mkali katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi Mtwara na Visiwa vya Unguja na Pemba na imewataka wananchi kuwa waangalifu.
Aidha mamlaka hiyo imesema kuwa sambamba na upepo huo mkali, pia kunatazamia kutokea mvua kali kwenye mikoa ya Rukwa, Mbeya ,Njombe, Mtwara, Ruvuma na Morogoro.
Taarifa ya mamlaka hiyo ilisema kwamba hali hiyo inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo wa hewa Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi na maeneo ya Mkondo wa Msumbiji.
Imesema kuwa mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka Pwani ya Somalia na misitu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
“Mamlaka inatahadharisha kuwa kuanzia leo hadi Januari 16, kunatarajiwa kujitokeza upepo mkali unaozidi kilometa 40 kwa saa pamoja na mawimbi makubwa zaidi ya 2.0.
Kutokana na hali hiyo tunawatahadharisha watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hatarishi kuchukua tahadhari,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.
Mamlaka hiyo imesema kuwa kiwango cha mvua kinatarajiwa kuongezeka hadi kufikia kiwango cha milimita 50 kwa saa 24 ikiwa ni wastani wa asilimia 60.
“Hata hivyo mamlaka inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo pale inapobidi, lakini tunasisitiza kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari,” imesema taarifa hiyo.
Tahadhari hii imekuja wakati Watanzania bado wanakumbuka nyingine iliyotolewa ndani ya wiki mbili zilizopita na siku chache baadaye vyombo viwili vya abiria vilivyokuwa vikisafiri Bahari ya Hindi kupata ajali na kusababisha vifo vya watu tisa.
Ajali zote mbili zilitokea Januari 5 mwaka huu, moja ikitokea karibu na eneo la Visiwa vya Mafia na nyingine eneo la Nungwi lililopo kati ya Unguja na Pemba.
Ajali iliyotokea Nungwi iliihusisha boti ya Kilimanjaro II baada ya kukumbwa na dhoruba.
Aidha mamlaka hiyo imesema kuwa sambamba na upepo huo mkali, pia kunatazamia kutokea mvua kali kwenye mikoa ya Rukwa, Mbeya ,Njombe, Mtwara, Ruvuma na Morogoro.
Taarifa ya mamlaka hiyo ilisema kwamba hali hiyo inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo wa hewa Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi na maeneo ya Mkondo wa Msumbiji.
Imesema kuwa mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka Pwani ya Somalia na misitu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
“Mamlaka inatahadharisha kuwa kuanzia leo hadi Januari 16, kunatarajiwa kujitokeza upepo mkali unaozidi kilometa 40 kwa saa pamoja na mawimbi makubwa zaidi ya 2.0.
Kutokana na hali hiyo tunawatahadharisha watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hatarishi kuchukua tahadhari,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.
Mamlaka hiyo imesema kuwa kiwango cha mvua kinatarajiwa kuongezeka hadi kufikia kiwango cha milimita 50 kwa saa 24 ikiwa ni wastani wa asilimia 60.
“Hata hivyo mamlaka inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo pale inapobidi, lakini tunasisitiza kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari,” imesema taarifa hiyo.
Tahadhari hii imekuja wakati Watanzania bado wanakumbuka nyingine iliyotolewa ndani ya wiki mbili zilizopita na siku chache baadaye vyombo viwili vya abiria vilivyokuwa vikisafiri Bahari ya Hindi kupata ajali na kusababisha vifo vya watu tisa.
Ajali zote mbili zilitokea Januari 5 mwaka huu, moja ikitokea karibu na eneo la Visiwa vya Mafia na nyingine eneo la Nungwi lililopo kati ya Unguja na Pemba.
Ajali iliyotokea Nungwi iliihusisha boti ya Kilimanjaro II baada ya kukumbwa na dhoruba.
No comments:
Post a Comment