23/08/2008 – 23/08/2013
Baba
yetu mpendwa, leo tarehe 23/08/2013
unatimiza miaka mitano (5) tangu
utwaliwe na Bwana mwaka 2008.
Sisi
wanao Tony, Ipyana, Ivan na Irene, mama yetu Esther Victoria, wajukuu zako
(Ben, Lulu, Baraka, Dan, Vicky, Milka & Vicent), wakwe zako pamoja na ndugu
na wanaukoo wote bado tunakukumbuka kwa Busara na Upendo wako.
Tunajua
kuwa kimwili haupo nasi ila tunaamini kuwa kiroho upo nasi. Tunaendelea kujivunia na kuyaenzi mema
uliyotufundisha enzi za uhai wako.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu
ailaze roho yako mahali pema peponi. AMEN.
No comments:
Post a Comment