Pages

Monday, July 29, 2013

WAZIRI NCHIMBI AJIBU HOJA ZA WASHIRIKA WA KONGAMANO LA AMANI, CHUO KIKUU DSM - JANA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk.t Emmanuel Nchimbi akijibu hoja mbalimbali za washiriki katika kongamano la amani na usalama wa taifa kwa miaka 50 ijayo.  Kongamano hilo lilifanyika  katika ukumbi wa mikutano wa Nkrumah uliopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).  Waziri Nchimbi amesisitiza kuwa watakaotaka kufanya maandamano ya aina yoyote ni LAZIMA wafuate sheria za nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akiandika maelezo ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Slaa, wakati alipokuwa akichangia mada juu ya mustakabali wa amani na usalama wa taifa kwa miaka 50 ijayo. Kongamano hilo lilifanyika jana katika ukumbi wa Nkrumah uliopo UDSM.

Waziri Nchimbi (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu mara baada ya kumalizika kwa Kongamano hilo lililofanyika jana katika ukumbi wa Nkrumah jijini Dar es Salaam.

Waziri Nchimbi (wa pili kushoto) akifurahi jambo wakati alipokuwa akizungumza na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa mara baada ya kufungwa kwa Kongamano hilo la Amani na usalama wa taifa kwa miaka 50 ijayo.

No comments: