Pages

Thursday, March 28, 2013

MBUNGE WA CHAMBANI AFARIKI DUNIA


w
Baadhi ya Maofisa wa Ofisi Ndogo ya Bunge wakimsaidia kwa kumbeba Mbunge wa Chambani Bw. Salim Hemed Khamis mara baada ya kuanguka ghafla hapo jana jijini Dar akiwa katika vikao vya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu ya haraka.
 
Mbunge wa Chambani-Pemba, Kisiwani  Zanzibar Salim Hemed Khamis ambaye jana aliugua ghafla wakati wa Kikao cha Kamati ya Bunge ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ofisi ndogo jijini Dar es Salaam amefariki.

Khamis, mara baada ya kuugua ghafla alisaidiwa na Wabunge wenzake na Maofisa wa Bunge na kukimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa matibabu na mchana huu  amefariki dunia.
 
Taratibu za kuusafirisha mwili wa Marehemu kuelekea Pemba kwa mazishi zinafanyika.



Kwa hisani ya  Father  Kidevu Blog

No comments: